Nani lyrics

  2024-06-28 01:33:12

Nani lyrics

(Mocco)

Asubuhi kumekucha

Wingu limetanda

Na mvua yata kunyesha

Na uko mbali mama

Maji takitiririka

Oh baridi itanishika

We ndo chanda chema

Uhakika unanikatisha tamaa

Utaambiwa binadamu

Ah kila mmoja ana mapungufu yake

Sijui nilipoteleza mama

Si ungeniambia

Nimemiss tabasamu

Kutwa kucha

Picha kummezea mate

Yangu fimbo umeibeza

Ah katu hautaki kuitumia

Labda hesabu za kutoa

Mi niligawanya baby unisamehe

Na ile hasi nikafanya chanya

Baby unisamehe

Na hata emoji za kulia

Nazo kutumia nazo zikome

Japo nipate furaha

Ah huruma unionee

Maana hii hali, hata haifichiki

Kutwa wima cha mpingo, kisiki

Maana hata nikiona michezo ya njiwa

Ah huwa naitamani

Kama si wewe

Nitampenda nani?

Nitampenda nani?

Nitampenda nani

Nani nitampenda

Nitampenda nani?

Nitampenda nani?

Nitampenda nani

Nani nitampenda aah

Eh penzi usifanye kwa chombo cha usafiri

Ikawa umeshuka uje utanikatili

Nitakuwaga mental Niko dhahari

Si unasikia

Penzi la dhati daima la wawili

We fanya na urudi lisiwe batili

Ka wafanya kusudi ni ukatili

Mi naumia

We ndo yangu hifadhi

Labda nilikosea msimbo

Kweli kupenda kazi

Wangu umegeuka fimbo o

Mi ndo lako koroboi

Lile lisilo zima

Aha si ulisemaga hauchomoi

Kumbe imani ulinipima ah

Pia ulisema haudonoi

Wameiteka mazima

Ahaa simung'unyi sikohoi

Sina vyangu nimechina

Maana hii hali, hata haifichiki

Kutwa wima cha mpingo, kisiki

Maana hata nikiona michezo ya njiwa

Ah huwa naitamani

Kama si wewe

Nitampenda nani?

Nitampenda nani?

Nitampenda nani

Nani nitampenda

Nitampenda nani?

Nitampenda nani?

Nitampenda nani

Nani nitampenda aah

  • Artist:Ibraah
  • Album:Steps (EP) (2020)
Ibraah more
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili, English
  • Genre:
  • Official site:
  • Wiki:
Ibraah Lyrics more
Excellent recommendation
Popular