Bwana umeinuliwa Katika kiti chako cha enzi lyrics

  2024-07-01 08:50:08

Bwana umeinuliwa Katika kiti chako cha enzi lyrics

Bwana Umeinuliwa katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Maserafi, wako mbele zako Mungu uu

wazikabithi heshima zako mbele zako,

Wanalia mtakatifu, ni wewe Mungu

Mtakatifu mtakatifu, ni wewe Mungu

Bwana Umeinuliwa katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Makerubi pia wako mbele zako ooh,

hata nao wazikabithi heshima zao

Wanazivua taji zao za dhahabu uuh,

wakiinama, mtakatifu ni wewe Mungu.

Bwana Umeinuliwa katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Wazee wale ishirini na wanne, eeh,

hata nao wazikabidhi heshima zao,

Wanainama, mtakatifu ni wewe Mungu uu,

mtakatifu, mtakatifu ni wewe Mungu.

Bwana Umeinuliwa aa, katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Viumbe wale walio hai ii,

hata nao wazikabithi heshima zao.

Wapeperusha, mabawa yao mbele zako, ooh,

wajifunika, mtakatifu ni wewe Mungu

Bwana Umeinuliwa aa, katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Nafsi yangu naiinua mbele zako ooh,

Naungamana na hilo jeshi la mbinguni,

mataifa yote nayo yajue, eeh,

ya kwamba wewe, wewe mungu ni mtakatifu

Bwana Umeinuliwa aaah, katika kiti chako cha enzi

Bwana Umeinuliwa aah, katika kiti chako cha enzi

Swahili Worship Songs more
  • country:
  • Languages:Swahili, Chewa
  • Genre:
  • Official site:
  • Wiki:
Swahili Worship Songs Lyrics more
Excellent recommendation
Popular