Dume Suruali

  2024-06-02 20:02:29

Dume Suruali

Vanessa Mdee

We ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami

Kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami

Hudat hudat hii ni salam na ufahamu

Kama unauza mapenzi siyo kwa binamu

Huna haja ya kusubiri hii ni hukumu

Hakuna kitu utapata utangoja kama askari wa zamu

Dume suruali, dume kaptula

Shauri zako ilimradi sipati hasara

Usione utani me sihongi hata kwa ishara

Utaniambia nini mpaka unigeuze fala

Kwanza nasikia hongo zinaleta mkosi...

Sentano yangu hugusi hata ukiongea kidosi

Yabaki mapenzi tusileteane ujambazi

Hata upige sarakasi utachonga viazi

(Bahili kama nini!)

Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada, hunitakii mema

Vanessa Mdee

We ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami

Kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami

I want that Gucci, Fendi, spend it on a girl like me

My name is Vee Money, money, spend it on a girl like me

Nihonge nanunua nini kwa nini yaani!

Kuna kipi nisichokijua ina TV ndani?

Usiulize n’takupa nini dada piga moyo konde

Viuno vingi kama mwali wa kimakonde

Usipende hela kama mfuko

Au fanya unavyofanya upate zako

Vishawishi vingi binti sema na moyo wako

Na ujifunze pesa zinauza utu wako

Tajiri mtata kama Salah

Zipo ila sitoi sobe hili me ni balaa

Unapenda hela zangu nami nazipenda pia

Kila mtu abaki na zake bye baby, tutaongea

(Mwanaume wa hivyo wa nini sasa!)

Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada, hunitakii mema

Vanessa Mdee

We ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami

Kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami

I want that Gucci, Fendi, spend it on a girl like me

My name is Vee Money, money, spend it on a girl like me

Aje aje ajee me mtoto fulani ghali

Nihonge gari, ma sweet sweet baby

Wanna see you today, unipeleke party

Aje aje ajeee njoo nikupe TBT

Siyo kwa enzi ya Magufuli

Zali ilikuwa long siku hizi hakuna la mentali

Nikikuhonga na ukiniacha nitakujia usingizini

Naepusha shari matatizo yote ya nini

Hakuna kipya chini ya jua

Hata nisiyoyafanya nishayasikia

Ningekuwa mhongaji ningeshafulia wangu

Mademu wangu wa zamani wote wangekuwa maadui zangu

(Mwanaume hovyo wewe!)

Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada, hunitakii mema

(Baki na hamu zako!)

Vanessa Mdee

We ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami

Kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami

I want that Gucci, Fendi, spend it on a girl like me

My name is Vee Money, money, spend it on a girl like me

[Vanessa] Baba bure huyu!!!

[MwanaFA] Hata pantoni lina staff

[Vanessa] Unamwambia nani sasa!

Unamwaaambia nani sasa!

MwanaFA more
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili
  • Genre:Hip-Hop/Rap
  • Official site:
  • Wiki:
MwanaFA Lyrics more
MwanaFA Featuring Lyrics more
Excellent recommendation
Popular