Iyena lyrics

Songs   2024-07-02 09:24:27

Iyena lyrics

Hmm, ah leo chereko chereko mwanenu nimekuwa

Zile kuringa mideko itapungua

Asante mama, ulinifunza nkajua

Baba kasema kuomba mwiko raha ya chumvi kununua

Tena si kwa nazi si hirizi za waganga

Kwa baraka za baba na mama tu na dua

Waambie paparazi, pingamizi wenye viranga

Waliosema hayawi hayawi yamekuwa

Ooooh oh!

Iyena Iyena

Iyena Iyena

Iyena Iyena

Kwaheri tutaonana

Iyena Iyena (aai ooh)

Iyena Iyena (aai Iyeena)

Iyena Iyena

Ntawakumbuka sana

Oooh ndoa baraka ukipata ushukuru

Maana wanayoililia ni wengi sana

Kwetu talaka kuitoa ni kufuru

Nimefunzwa vumilia, niushinde ujana

Ili kesho mahususi kusudi wasinong'one

Embu nichumu niringe washushuke

Na hii pete ya harusi nakuvisha waone

Wakale sumu wavimbe wapasuke

[Diamond Platnumz & Rayvanny]

Eeh!

Ati nashika nanga nteke nsichomoke ndani

(Anameremeta)

Futa namba wablock vimada wa zamani

(Anameremeta)

Sio vijembe vya kanga waziwazi mambo hadharani

(Anameremeta)

Waliopanga mwenye nyumba kaja ndani

(Anameremeta)

Iyena Iyena (aah iyoyo)

Iyena Iyena (aah eeeh)

Iyena Iyena

Kwaheri tutaonana (oh, kwaheri Baba, Mama)

Iyena Iyena (Iyeeena)

Iyena Iyena (aah eeh)

Iyena Iyena

Ntawakumbuka sana

[Rayvanny]

Imefika tamati tulisubiri kitambo

Leo samaki kanasa kwenye chambo

Pongezi kwa kamati yanavutia mapambo

Napata picha safi litanikoma bundle

Mwanamke usafi gaga kulisugua

Mume akirudi sharti viatu kumvua

Kitandani marashi massage kumchua

Kisha anza sayansi, viuno kutengua

Mambo ya kuzima taa si mahaba ni kuwanga

Washa japo ka mshumaa mumeo aone shanga

[Rayvanny]

Eeeh!

Makeup kinanda kaka suit kama mbunge

(Anameremeta)

Mulo changa muda kujipooza na punje

(Anameremeta)

Momo ndani, Shivo amekuja na Fumbwe

(Anameremeta)

Kula chanda ukishiba ruksa kafunge

(Anameremeta)

Iyena Iyena (aah iyeee)

Iyena Iyena (aah iyoyo)

Iyena Iyena

Kwaheri tutaonana (eh, kwaheri Baba, Mama)

Iyena Iyena (Iyeee)

Iyena Iyena (hmm)

Iyena Iyena

Ntawakumbuka sana

[Diamond Platnumz & Rayvanny]

Saa nataka kusasambua (sasambu)

Me nasasambua (sasambu)

Abidadi nasasambua mimi (sasambu)

Sasambua tuone

Mguu moja juu (sasambu)

Usishushe chini (sasambu)

Cheza jitazame (sasambu)

Sasambua tuone

Aisha Kimobitel (sasambu)

Nipe za Balotelli (sasambu)

Nyonga kibaiskeli (sasambu)

Sasambua tuone

Akaa kama unashika ukuta (sasambu)

Ifanye unashusha (sasambu)

Taratibu zungusha (sasambu)

Sasambua tuone

Sasambu, sasambu, sasambu

Sasambua tuone

Kama unawasha bajaji (sasambu)

Imwagie na maji (sasambu)

Tuwakomeshe vizazi (sasambu)

Sasambua tuone!

Diamond Platnumz more
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili, English, English (Nigerian Pidgin), Lingala
  • Genre:Folk
  • Official site:
  • Wiki:
Diamond Platnumz Lyrics more
Diamond Platnumz Featuring Lyrics more
Excellent Songs recommendation
Popular Songs
Artists
Songs